Ndege aliyesafiri kutoka Finland hadi Uganda

Ndege huyo alikuwa na pete yenye maelezo kumhusu
Ndege mmoja ambaye inaaminika alitoka nchini Finland amepatikana katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda.
Ndege
huyo aina ya Osprey kwa sasa anatunzwa na maafisa wa kituo cha
kuwahudumia wanyama cha Uganda Wildlife Education Centre (UWEC).
Isaac Mujaasi, afisa wa mauzo na mawasiliano katika UWEC, ameambia BBC kwamba ndege huyo alikuwa ameumia katika mabawa yake baada ya kugongwa na ndege iliyokuwa inapaa.
- Tai wa Israel aliyedhaniwa kuwa jasusi sasa huru
Afisa huyo hata hivyo amesema ni kawaida kwa ndege kuhama kutoka Ulaya, hasa wakati wa majira ya baridi na kukimbilia maeneo yenye joto.
Leave a Comment