Siri mkataba wa Lugumi sasa kuanikwa hadharani
Siku moja baada ya Spika wa bunge Job Ndugai kutangaza mkataba tata kampuni ya Lugumi Interprises Limited na jeshi la polisi litajadiliwa mwezi ujao mjini Dodoma kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za serikali PAC imesema imepata nguvu ya kuliweka wazi zaidi kwa umma
Aidha, PAC imesema leo inakaa kuandaa ripoti ambayo itaiwaiwasilisha katika mkutano ujao huo wa bunge.
Katika mahojiano na kituo cha Azam televisheni jijini Dar es Salaam juzi, Ndugai alisema sakata hilo litajadiliwa katika mkutano wa Bunge utakaoanza Septemba 6.
Katika mahojiano na kituo cha Azam televisheni jijini Dar es Salaam juzi, Ndugai alisema sakata hilo litajadiliwa katika mkutano wa Bunge utakaoanza Septemba 6.
Kampuni hiyo ilikuwa inatekeleza mradi wenye
thamani ya Sh. bilioni 37 wa kusimika mfumo wa utambuzi wa alama za
vidole kwenye vituo vya polisi nchi nzima.
Katika mahojiano na Nipashe jana, Makamu
Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilary, alisema kuwa kutokana na uzito wa suala
hilo, leo wanaanza kukaa kuandaa ripoti ambayo wataiwasilisha bungeni
ili wananchi wafahamu ambacho kamati ndogo ya PAC ilikibaini baada ya
kutembelea vituo vya polisi ambavyo mfumo huo ulikuwa unasimikwa.
"Tamko la Ndugai limetupa nguvu ya kuueleza
umma yale tuliyoyabaini. Kamati ina maazimio yake tutayaweka wazi kwa
umma wakati wa vikao vya mkutano ujao wa bunge," Hilary alisema.
Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ambaye
hakutaka jina lake litajwe gazetini kwa maelezo kuwa si msemaji wa
kamati, alisema walibaini 'uozo' katika utekelezaji wa mradi huo lakini
walikosa nafasi ya kuueleza baada ya bunge kutoa tamko na kuifanya
kamati ionekane haina meno.
"Kamati ilikosa nafasi ya kuueleza umma ilichokibaini baada ya Dk. Tulia Ackson kutoa tamko la bunge kuhusu mradi huo,"
alisema mjumbe huyo.
alisema mjumbe huyo.
Juni 30 wakati wa kuliahirisha bunge, Dk.
Ackson aliitaka serikali kukamilisha mradi huo ndani ya miezi mitatu
kuanzia siku hiyo.
Hilary ambaye pia ni Mbunge wa Sumbawanga
Mjini (CCM), alisema kamati ilikuwa imepanga kupitia ripoti za hesabu
mbalimbali za mashirika ya umma lakini italazimika kupangua ratiba yake
ili kukamilisha ripoti ya sakata hilo.
Aprili 23, PAC iliunda kamati ndogo ya watu
tisa iliyoongozwa na mwenyekiti Japahet Hasunga ambaye ni mbunge wa
Vwawa (CCM), ili itembelee vituo vya polisi Tanzania Bara na visiwani
kuchunguza utekelezaji wa mradi huo.
PAC ililazimika kuunda kamati hiyo ndogo baada ya kushindwa kupata ufafanuzi wa kina kutoka kwa Katibu Mkuu wa
Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Projest Rwegasira na maofisa wengine wa Jeshi la Polisi iliyowahoji kwenye ofisi za Bunge Aprili 20 kuhusu sakata hilo.
Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Projest Rwegasira na maofisa wengine wa Jeshi la Polisi iliyowahoji kwenye ofisi za Bunge Aprili 20 kuhusu sakata hilo.
Baada ya kumaliza uchunguzi wake, kamati ndogo
ya PAC yenye wajumbe (wabunge) watano wa CCM na wanne kutoka upinzani
(vyama vya CUF na Chadema vikitoa wajumbe wawili kila kimoja), ilirejea
bungeni mjini Dodoma Mei 24.
Mwanzoni mwa Aprili, PAC ilieleza kuwa kampuni
ya Lugumi ililipwa Sh. bilioni 34 na Jeshi la Polisi ili kufunga vifaa
hivyo katika vituo 138 vya polisi nchini, lakini ni vituo 14 tu ndivyo
vilivyokuwa vimefungiwa, licha ya kulipwa fedha hizo ambazo ni sawa na
asilimia 90 ya malipo yote ya kazi hiyo.
Ulipaji wa asilimia 90 ya malipo ya kandarasi kabla ya kukamilika kwa kazi ni kinyume na sheria ya manunuzi ya umma.
Leave a Comment