Tuzo ya benki bora mitandaoni Tanzania 2016 imekwenda kwa Bank ABC
Jitihada za BancABC katika ubunifu
kuendeleza na kufanikisha usalama wa miamala matandaoni Tanzania
imetambuliwa kwa tuzo ya ViISA kuthibitisha ubora wa huduma yake
mitandaoni.
Mkuu wa kitengo cha wateja binafsi na
wafanyabishara wadogo Joyce Malai alithibitisha taarifa hiyo
alipozungumza na vyombo vya habari mapema katika makao makuu ya bank ABC
Dar es salaam.
“Tunafurahi kupokea tuzo hii licha ya
ushindani wa masoko uliopo, hii inaonyesha ni jinsi gani tumejidhatiti
kuhudumia wateja wetu na kuwarahisishia kufanya miamala ya kifedha,”
alisema Bi. Malai.
Akasema tena kwamba katika jitihada hizi za kuboresha miamala salama mitandaoni, mtu yeyote anaweza kumiliki kadi hii ya VISA bila kujali kama anayo akaunti ya BancABC au la.
Bi. Malai alifafanua kwamba kadi ya VISA ya BancABC ni rahisi kutumia kwani inamuhakikishia mteja ulinzi wa fedha zake na pia huondoa usumbufu wa kutembea na pesa taslimu.
Kadi hii inaweza kutumika kufanyia
miamala mbalimbali ya kifedha kama vile kulipia tiketi za ndege pia
kulipa posho na mishahara kwa wafanyakazi, kulipa ada za shule na
kujikimu kwa wanafunzi, mikopo na misaada kwa serikali na mengineyo.
Sasa kama hapo ulipo upo tayari kuichukua hii kadi
unatakiwa kwenda na kitambulisho halisi na kisha kujaza fomu
zinazopatikana katika tawi lolote la benki hii.
Wateja wanaweza kuweka fedha kwenye kadi
hii kwa kutumia huduma mbalimbali za kutuma pesa kama vile TIGOPESA,
AIRTELMONEY au M-PESA pamoja na benki nyingine zilizopo Tanzania.
Leave a Comment